Akina mama Idaya Salum, Violet Mkwawa na Mariam Abdu wanaofadhiliwa na shirika la Care International wakiuza vikapu maalum vya kuwekea maua vilivyotengenezwa kwa ustadi mkubwa kwa kutumia majani makavu katika maonyesho ya wakina mama wajasiriamali katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika viwanja vya mnazi mmoja leo.
Wageni kutoka Norway Anne kushoto na Graziella Van Den Bergh wa chuo kikuu cha Bergen University College wakijinunulia vitu mbalimbali wakati walipotembelea maonyesho ya akina mama yaliyofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja leo katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani




